KUWA NA VIPINDI VINGI VYA HEDHI

KUWA NA VIPINDI VINGI VYA HEDHI NA KUWA NA VIPINDI VICHACHE KWENYE HEDHI
POLYMENORRHEA & OLIGOMENORRHEA


Kwa kawaida mzunguko wa hedhi huchukua siku 21 mpaka 35 lakini wastani wa wanawake wengi huenda siku 28 kama inavyotumiwa katika vitabu vingi.

Kama mwanamke anaenda mzunguko wa siku 21 basi katika mwaka wenye siku 365 ataenda mizunguko 17 (365/21=17) na yule mwenye mzunguko wa siku 35 atakuwa na vipindi 10 vya hedhi( 365/35=10) katika mwaka

Hivo mwanamke anayeenda wastani wa siku 28 anakuwa na mizunguko 13, na ikiwa mwanamke anaenda hedhi zaidi ya vipini 17 au mzunguko chini ya siku 21 katika mwaka basi mwanamke huyo huitwa aneenda mizunguko mingi ya hedhi au kiingereza polymenorrhea. Na endapo mwanamke anaenda hedhi chini ya vipindi 10 katika mwaka au zaidi mzunguko unaochukua zaidi ya siku 35, basi huyu huitwa anamizunguko michache ya hedhi. Polymenorrhea huweza kusababishwa na matatizo mbalimbali katika mfumo wa uzazi au mfumo wa vichochezi mwili(hormone

Nini husababisha kuona vipindi vingi katika mwezi(polymenorrhea)?

Kuna sababu mbalimbali, zipo sababu za kawaida zisizo za hatari kama msongo wa mawazo, mazoezi makali, matumizi ya dawa mbalimbali na matatizo ya mwanamke akiwa anaanza kuacha kuona siku zake. Sababu zingine ni matatizo/magonjwa kwenye mfumo wa uzazi. Baadhi ya sababu hizo zimeelezewa hapo chini.

  • Kuharibika/kutokuwepo kwa uwiano wa vichochezi mwili

Hili linaweza kusababishwa na mambo mbalimbali kama vile chakula unachokula endapo hakina virutubisho vya kutosha, kubadili chakula, kubadili mfumo wa maisha ya kila siku na kubadili ratiba ya kulala kila siku.

Tatizo hili huweza kuwa kubwa na kusababisha mwanamke kuongezeka uzito kubadilika tabia na hulka yake kuhalibika, ni vema kupata ushauri na msaada wa kiafya endapo hili litatokea.

  • Kujipandikiza nje ya kizazi kwa chembe za ukuta wa ndani ya mfuko wa kizazi(endometriosis)

Chembe za ndani ya uzazi huweza kujipandikiza katika mayai, nje ya misuli ya mfuko wa kizazi, kwenye mirija ya kupitisha mayai n.k. kuwepo kwa chembe hizi nje ya kizazi husababisha kuvuja kwa damu ya hedhi ndani na madhara yake ni michomo na kushikamana kwa organi ndani ya nyonga. Mwanamke anapata dalili za  maumivu makali wakati wa hedhi pamoja  kuwa na vipindi vingi vya hedhi katika mwaka.

  • Vimbe kwenye ukuta wa uzazi(uterine Fibroids)
Kuwepo kwa vimbe ndani ya ukuta wa kizazi huufanya ukuta unaotengenezwa kila mwezi (kwa ajili ya kupokea yai endapo limechavunshwa)kutokuwa imara na hivo husababisha ukuta huu kuvunjika kabla ya mzunguko kukamilika na mwanamke anakuwa na vipindi vingi vya hedhi.

  • Kuanza kukoma kwa Mzunguko wa Hedhi (perimenopause)
Kukoma kwa mzunguko wa Hedhi ni jambo la kawaida kwa mwanamke anapofikia umri zaidi ya miaka 45. Dalili zake ni kama kutokwa na jasho wakati wa usiku, kubadilika kwa tabia au hulka ya mtu na kuwa na vipindi vingi vya hedhi katika mwezi. matatizo haya huletwa kutokana na mabadiliko ya vichochezi mwili(hormone) yanayotokea kwa mwanamke anapokuwa anazeeka.

  • Magonjwa ya zinaa 
Ugonjwa wa chlamydia  na kisonono(Gonorrhea) ni mojawapo ya magonjwa  yanayosababisha kutoka kwa uchafu ukeni, maumivu ya tumbo chini ya kitovu na mgongoni pamoja na kubadilika kwa mfumo wa hedhi kama kuwa na vipindi vingi vya hedhi. Nimuhimu kwenda kumuona daktari endapo unapata dalili hizi kwa ajili ya matibabu

Ni yapi matibabu ya tatizo hili?

Tatizo la kuwa na vipindi vingi vya hedhi huweza kutibiwa endapo sababu imejulikana ni nini, kama tatizo ni msongo wa mawazo, dawa za mpango wa uzazi,mazoezi makali, uzito na mengine, matibabu yake ni kukabiliana na mambo hayo. Na endapo utaenda hospitali basi utapimwa vipimo mbalimbali na kutibiwa tatizo lako.

Kumbuka ni vema kwena hospitali kwa mtaalamu wa afya ili kupata ushauri na matibabu ya tatizo lako.
Endapo unasumbuliw na tatizo hili waweza kuwasiliana nasi kupitia barua pepe na namba za simu hapo chin

No comments