TATIZO LA KIPARA KWA VIJANA (ANDROGENETIC ALOPECIA).

Katika  miaka  ya  hivi  karibuni, suala  la  upara  ( baldness )  linatajwa  kuwasumbua  vijana  wengi  wa  kiume. Miaka  ya   tisini  kurudi  chini  ilikuwa  ni aghalabu  sana  kumuona  kijana  wa  miaka  25  akiwa  na  upara,  na  mara  nyingi  suala  la  upara  lilikuwa  likihusishwa  na  uzee,lakini  leo  hii   hali  ni  tofauti  sana, kwani  kuna  idadi  kubwa  sana   ya  vijana  wa  kiume  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  25  hadi 45  wana okabiliwa  na  tatizo  la  upara. Pamoja  na  kwamba,  kutokuwa  na  nywele  hakuwezi  kukamfanya  mwanadamu  akashindwa  kuishi, lakini  katika  dunia  ya  sasa  ya  mitindo  na  utandawazi  kuwa  na  upara  ni  jambo  linalo  wapa  shida  sana  wahusika. 
Tatizo hili linajulikana kitaalamu kama hair Loss and Male pattern baldness.


NINI HUSABABISHA TATZO HILI
tatzo hili linasababishwa na vitu viwili ambavyo ni matatizo ya hormones na kurithi kutoka kwa wazazi(kijenetiki),
Kwa wanaume hormone za kiume (androgens) zina kazi ya kufanya mtu abalehe na kutokea kwa mabadiliko ya mwili baada ya balehe. Mfano kukua kwa uume,mabadiliko ya sauti na ukuaji wa nywele na ndevu.

            Sababu nyingine ni Lishe  mbovu,Ukosefu  wa  Vitamin  B6 na  Kuwa  na  stress,  mfadhaiko  na  mshuko  wa  moyo  kwa  muda  mrefu
L
Kwa nn tatizo hili linaitwa male pattern baldness
Tatzo hili linaitwa pattern baldness kwa sababu mtu mwenye tatzo hili nywele zake hupukutika kwa kufata mlolongo au mstari,kama inavyoonekana katika mchoro huo hapa chini.aina ya kwanza (type 1) ni kiasi kidogo cha nywele kilichotoka kwa mbele.hadi kufikia stage ya tano (V) unaweza kuona ni sehemu kubwa imepoteza nywele.
Norwood-Hamilton scale
MATIBABU
Upara hauathiri afya mtu,
Umekua ukitolewa ushauri mbali mbali kuhusu dawa za upara.lakini dawa zilizoonesha matokeo katika kutibu tatzo hili ni mbili ambazo ni

1.minoxidil hii hufanya kazi kwa kuchochea kuota na kukua kwa nywele.dawa hii inapakwa sehemu iliyoathirika.
2.finasteride dawa hii pia inasaidia katika.ukuaji wa nywele.dawa hii yenyewe inakua katika mfumo wa vidonge.


Kumbuka kabla ya kutumia dawa yoyote fika hospiali upate ushauli wa daktari.

No comments