- utumiaji wa mionzi ya x-ray kwenye matibabu ya saratani mbalimbali(radiotherapy) zinazotokea kwenye maeneo ya kichwa na shingo ambapo tezi za mate zinaweza kudhurika.
- matatizo ya saikolijia kama vile sonona.
- Uvutaji wa sigara
- Magonjwa kama UKIMWI,kisukari (poorly controlled diabetes)
- upungufu wa maji mwilini,
- matumizi ya madawa ambayo hutumika kutibu magonjwa mbalimbali (mf.antihistamines,decongestants,antihypertensives and antidepressants)
dalili zake zikoje


- Kuchanika na kuvimba kwa mdomo(splitting and cracking of lips)
- Kuwa na harufu mbaya mdomoni
- Kushindwa kutafuna pia kumeza chakula hasa vyakula vikavu
- Kukosa ladha ya chakula
- Kuchanika na maumivu kwenye ulimi,mashavu kwa ndani na pembeni ya midomo
- Kuongezeka kwa matatizo ya fizi na kutoboka kwa meno
- Kushindwa kuongea vizuri kutokana na kinywa kuwa kikavu
- Kuongezeka kwa hamu ya kunywa maji hususani usiku.
- Maambukizi ya fangasi za mdomo



matibabu yake ni yapi?
Matibabu
ya kinywa kuwa kikavu isivyo kawaida yamejikita hasa katika dalili
zinazoonyeshwa na hali hii. Kuongeza uzalishaji wa mate katika kinywa
kama vile kunywa maji mengi,kupunguza dozi ya dawa au kubadilisha kama
inawezekana,kutumia dawa ya kuongeza uzalishaji wa mate kwa mfano
pilocarpine(sialagogues),kuwa na kinywa kisafi


No comments