Dalili
na viashiria kama kuchanganyikiwa, degedege na kupoteza fahamu huhitaji
matibabu ya haraka. Kugunduliwa mapema na kupata matibabu huweza
kuokoa maisha ya mtoto.
Dalili
Mtoto
mwenye tatizo la reyes mara nyingi kiwango cha sukari wmilini hushuka
wakati kiwango cha kemikali za ammonia na hali ya aside ya damu
huongezeka, wakati huo huo ini huvimba na hukusanya kiwango kikubwa cha
mafuta- hukaliwa na kiwango kikubwa cha mafuta. Uvimbe unaweza kutokea
pia kwenye ubongo, na hupelekea kupata degedege na kupoteza fahamu.
Dalili
za reyes syndrome hutokea mara nyingi siku ya 3 hadi 5 baada ya kupata
maambukizi ya virusi wa tetekuwanga mafua ama maambukizi kwenye mfumo wa
juu wa hewa kama mafua.
Daliliz a awali za reyes syndrome
-
Watoto walio chini ya umri wa miaka 2 hupata dalili za
-
Kuhara
-
Kupumua kwa haraka
Dalili za ziada
-
Hali ya ugonjwa inapozidi kuwa mbaya dalili na viashiria na viashiria vinavyojitokeza huwa mbaya zaidi kama;
-
Mtoto kulialia, kuwa mkali au tabia zisizo za kawaida
-
Kuchanganyikiwa, kutotambua mata, kuwa mkali au tabia zisizo za kawaida
-
Kuchanganyikiwa, kutotambua mazingira na kupata ndoto
-
Kuchoka au kupooza kwa miguu na mikono
-
Degedege
-
Mwili kulegea sana
-
Kupungua kwa ufahamu
Wakati gani wa kumwona daktari
Kugunduliwa
mapema na kupata matibabu ya tatizo la reyes syndrome huweza kuokoa
maisha ya mtoto, kama unashuku mwanao ana tatizo hili basi mwahishe mara
moja hospitali
Visababishi
Visababishi
halisi vya tatizo la reyes syndrome huwa havifahamiki, ingawa kuna
mambo kadhaa huchangia katika usababishaji wa tatizo hili. Tatizo hili
huonekana kuamshwa na matumizi ya dawa ya aspirini kutibu maambukizi ya
virusi sana sana mafua na tetekuwanga kwa watoto ama vijana wadogo ambao
wanatatizo la uchakataji wa mafuta kwenye ini.
Matatizo
ya uchakataji wamafuta kwenye ini huwa ya aina nyingi na hurithiwa,
tatizo hili huambatana na kushindwa kwa uvunjwaji wa mafuta kwa sababu
vimeng’enya vinakosekana au havifanyi kazi ipasavyo. Kipimo cha ugunduzi
kinahitajika kugundua kama mwanao ana tatizo la uchakatuajiw a mafuta.
Vihatarishi
vihatarishi vifuatavyo vikitokea kwa pamoja siku zote huweza kuongeza hatari ya kupata tatizo la reyes syndrome.
Matumizi ya asipirni kwa mgonjwa mwenye virusi kama mafua, tetekuwanga au maambukizi ya mfumo wa juu wa hewa.
Kuwa na tatizo kwenye ini la uchakataji hafifu wa mafuta
Madhara
Vipimo na matibabu
Hakunakipimo maalumu cha kugundua tatizo la reyes syndrome. Ingawa vipimo vifuatavyo vinaweza kufanyika viwili ama kimojawapo.
-
Kipimo cha kuchukua maji wkenye uti wa mgongo
-
Kipimo cha kuchukua kinyama kwenye ini
-
Kipimo cha CT
-
Kipimo cha ngozi
Matibabu
Matibabu
ya reyes syndrome hufanyika hospitali. Mgonjwa mwenye hali mbaya zaidu
hutibiwa kwenye chumba cha uangalizi makini yaani ICU. Wafamnyakazi wa
hospitali watakuwa wakipima shinikizo la damu la mtoto kwa karibu sana
na vipimo vingine vya uhai. Matibabu huwa pamoja na;
-
Kuwekewa maji kenye mishipa
-
Madawa ya kupunguza maji mwilini-mdawa haya hupunguza uvimbe na shinikizo kichwani kwa njia ya kukojoa.
-
Madawa ya kuzuia kutokwa damu- kutokwa damu kutokana na kuharibiwa na ini hutibiwa kw akutumia vitamini K, kuongezewa giligili ya plasma na chembe sahani.
-
Kama mtoto anapata shida ya kupumua basi atawekewa mashine ya kumsaidia kupumua
No comments