Utandu mweupe(oral thrush) unakuwa kama maziwa kwenye kinywa cha
mtoto ni infection inasababishwa na fungus wanaoitwa candida albicans.
Utandu(thrush) huo unamwadhiri mtoto sehemu ya ulimi ,kuta za
mashavu kwa ndani na ufizi linawapata haswa watoto wachanga waliotoka
kuzaliwa mpaka miezi 2-4,pia inawapata watoto wakubwa na watu wazima
pia.
Sababu ya mtoto kupata utandu kinywani ni nini?
Candida fungus wanapoongeka kuwa wengi mwilini ndio wanasababisha
mtoto kupata utandu kinywaji.candida fungus nao wanasababisha na haya
matatizo ndio wanakuja kuzalishwa wengi kwenye mwili wa mtoto
-
Hana kinga ya kutosha mwilini na bado inajitengeneza ndio hapo inakuwa rahisi kwake kupata infection.
-
Mama alivyokuwa mjamzito au mtoto anapotumia dawa za antibiotic
anapunguza kinga ya mwili ndio mana inakuwa rahisi kushambuliwa.
-
Mtoto akitumia antibiotic inasababisha kupunguza kinga wa bacteria
-
Mama anaenyonyesha nae akitumia antibiotic inachangia mtoto kupata utando
-
Mtoto anaweza pata hili tatizo kipindi anapozaliwa kupitia uke wa mama
Dalili za utando (thrush)
-
Mtoto atalia wakati wa kunyonya au kula
-
Mtoto atapata vipele vidogo vidogo sehemu ya matako,mapajani (diaper rash)
-
Utandu mweupe usio futika hata ukifutwa sehemu za ufizi juu,kuta za mashavu na juu ya ulimi
4.Utando unaweza ambatana na rangi nyekundu kama damu kwa mbali
5.Kunuka mdomo wa mtoto
Tiba
Utajuaje kama ni utando wa maziwa au infection? ,safisha mikono yako
vizuri kwa maji safi na sabuni,jaribu kuifuta na kidole uone kama
inaweza toka ,iwapo ikatoa ujue hayo ni maziwa tu ndio yametengeneza
utandu,isipo toka ujue ni infection.
Utandu huo unaweza mletea mtoto vidonda pia mdomo ,utajua wakati wa
kunyonyesha au kumpa kuchupa ya chuchu kunyoa anashindwa na kulia
kutokana na maumivu anayopata,mpeleke hospital watamwandikia dawa ya
maji au gel atakayo tumia baada ya wiki 1 hapo utaona mabadiliko.Madhara
ya utando wa kinywa unaweza mletea mtoto nappy rash
Ushauri
Usafi ni muhimu sana kwa mtoto,mama hakikisha matiti yako unasafisha
vizuri sehemu ya chuchu kabla ujamnyonyesha ili tatizo lisijirudie
sababu infection inaweza hamia kwenye chuchu,hakikisha unaosha vizuri
chupa zake au pacifier (chuchu ya plastik) kama mnampa kuinyonya.
Unaweza mpa paracetamol kupunguza maumivu ili amudu kula chakula
(maziwa).Mama anae nyonyesha au mjamzito acha kutumia antibiotic
inapunguza kinga ya mtoto na yakwako pia, sio kila ugonjwa lazima utumie
antibiotic ni kali sana.
Tiba yake kwa mtoto ni ipi?mwanangu alipatwa na hali hii katumia dawa amemaliza ila tatizo linarudi tena
ReplyDeleteThanks
ReplyDeleteThanks
ReplyDelete