TATIZO LA MATEGE-Rickets

Matege ni hali ya mifupa kuwa laini na dhaifu, hali hii husababishwa na kuwepo kwa upungufu endelevu wa madini ya vitamini D kwa watoto.
Vitamini D huongeza ufyonzaji wa madini ya kalisium na phosphorua kutoka kwenye mfumo wa chakula-utumbo na kuingia kwenye damu. Upungufu wa vitamini D husababisha uwiano wa madini ya kalisium na phosphorus kuharibika na hivyo mifupa kuwa dhaifu na kupata tatizo la matege-rickets.

Kama upungufu wa vitamini D ama kalisiumu utasababisha matege, kwa kuongeza vitamin D ama Madini ya kalisium kwenye chakula huweza kunaweza kurekebisha tatioz la matege kwa mwanao. Matege kutokana na tatizo la kijeni-kuzaliwa nalo huwa vigumu kutibika na huhitaji matibabu ya ziada. Baadhi ya matatizo ya mifupa huweza kurekebishwa kwa njia ya upasuaji.

Dalili

Dalili za tatizo la rickets huwa pamoja ni

  • Kuchelewa kukua
  • Maumivu ya utu wa mgongo, kiuno na miguu
  • Misuli kuwa dhaifu

Kwa sababu tatizo la rickets huathiri chembe za ukuaji wa mifupa, mwisho wake husababisha matatizo ya mifupa kama

  • Kupinda kwa miguu kama upinde wa mvua
  • Viganja na magoti kuwa nene
  • Mifupa ya kwenye chuchu kutangulia mbele zaidi
  • Wasiliana na daktari wako endapo mwanao anaonekana kupinda miguu
     
Visababishi

Mwili wako unahitaji vitamin D ili kufyonza madini ya kalisiumu na phosphorus kwenye chakula kinachoingia tumboni. Tatizo la rickets huweza kutokea endapo mwanao anakosa  kiwango cha kutosha cha vitamini D au mwili wake unashindwa kutumia vema vitamin hii kutokana na matatizo katika chembe hai.

Upungufu wa vitamini D Unaweza kupata vitamin D kutokana na

Mwanga wa jua- ngozi huwa na uwezo wa kuzalisha vitamin D endapo itaanikwa kwenye jua haswa lile la asubuhi. Watoto walio kwenye nchi zilizoendelea hukaa kwa kiwango kidongo kwenye mwanga wa jua, na pia hukaa kwenye nyumba zenye vioo ambavyo haviruhusu kupitishwa kwa mwanga wa jua na hivyo kutopigwa na mwanga wa jua na kukosa vitamin D.

Chakula

Mafuta ya samaki, kiini cha mayai. Baadhi ya vyakula siku hizi vimeongezewa madini ya vitamini D kama vile maziwa, vyakula vya nafaka na vinywaji vya matunda. Watoto ambao hawapati vyakula hivi hupata tatizo la rickets

Tatizo la ufyonzaji
Baadhi ya watoto wamezaliwa na tatizo la kiafya linalozuia ufyonzaji wa vitamini D kama vile
  • Ugonjwa wa celiac
  • Ugonjwa wa Michomo kwenye mfumo wa chakula IBD
  • Ugonjwa wa cystic fibrosis
  • Matatizo ya figo

    Vihatarishi

  • Umri miezi 3 hadi 36 huwa hatarini kupata tatizo la rickets kwa sababu mifupa yao hukua haraka sana
  • Ngozi nyeusi- ngozi nyeusi huwa haipokei mwanga wa jua vema kuliko ngozi nyeusi hivyo huzalisha vitamin D kwa kiwango kidogo.
  • Mazingira- watu wanaoishi mazingira ya kaskazini mwa dunia hupata mwanga wa jua kwa kaisi kidogo na hivyo hutengeneza kiwango kidogo cha vitamini D.
  • Kuzaliwa kabla ya umri-njiti
  • Madawa ya kutibu kifafa- huwa na mwingilino katika utumiaji wa vitamini D kwenye chembe za mwili.
  • Kunyonya maziwa tu-maziwa ya mama huwa hayana kiwango cha kutosha kuweza kuimarisha mifupa. Watoto wanaonyonya maziwa ya mama tu wanatakiwa kupata matone ya vitamini D

    Madhara
  • Kushindwa kukua
  • Uti wa mgongo kupinda
  • Matatizo ya mifupa kufanyika vibaya
  • Matatizo ya meno
  • Kifafa



Vipimo na utambuzi

Daktari atamchunguza mwanao kwa kubonyehsa kwa kiasi kwenye mifupa ya mwanao kuangalia udhaifu na atatia umakini kwenye mifupa ya;

Kichwa- mtoto anaweza kuchelewa kufunga kwa utosi
Miguu-watoto wagodo huonekana  na miguu upinde kiasi, ila watoto wenye upungufu wa vitamini D huwa na upindi unaoonekana sana.
Kifua- huchomoza mbeleviganja
Magoti na viganja- huwa kubwa kuliko kiasi

Kipimo cha xray pia huweza kuonyesha udhaifu katika mifupa ya watoto

Matibabu

Matibabu ya dawa kama vitamini D na Madini ya kalisium. Fuata ushauri wa daktari wako kuhusu matumizi ya dawa hizo

Matibabu ya upasuaji- kama miguu imepinda kama upinde wa mvua, daktari anaweza kukushauri kutumia viatu ama vazi maalimu linaliweza kunyoosha miguu. Matatizo makubwa ya kupinda miguu huweza kutibiwa kwa njia ya upasuaji.

Kijikinga na upungufu wa vitamini D

Watoto wengi na vijana wanapata kiasi cha kutosha cha vitamini D kutoka kwenye jua. Vichanga na watoto wadogo kabisa huweza kukosa kiasi cha vitamini D kinachohitajika kwa sababu hawakai kwenye mwanga wa jua
Kama ndo hivyo basi hakikisha mwanao anapata kiasi cha kutosha cha vyakula vyenye vitamini D kama mafuta ya samaki, kiini cha yai au vyakula vya kusindikwa kama

  • Maziwa ya kopo
  • Nafaka
  • Maziwa
  • Juisi ya machungwa

Kwa sababu maziwa ya binadamu huwa na kiwango kidogo cha vitamini D watoto wote wanaonyonya tu wanahitaji kupata vitamini D kiasi cha 400IU kwa njia ya mdomo kila siku


No comments