USUGU WA VIMELEA DHIDI YA DAWA ZA ANTIBIOTIKI




Tatizo la kutumia vijiuasumu(Antibiotics) bila ya kupata vipimo na ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya limekua kubwa ambalo linasababisha madhara ya kiuchumi na uhai kutokana na kuzidiwa na vimelea vya ugonjwa ambavyo vinakua sugu kutokana na  matumizi mabaya ya dawa hapa nchini



 Dawa   za   Antibiotiki   ni   dawa   ambazo   zipo   kwenye   kundi   kubwalinalojulikana   kama  antimicrobials.  Antimicrobials  ni   dawa   ambazohutumika   kuua   au   kuzuia   ukuaji   wa   vimelea   vinavyosababishamagonjwa ya kuambukiza kwa binadamu na wanyama

Tafiti za Kimataifa zinaonesha kuwa kuna ongezeko kubwa duniani lamatumizi ya dawa za  antibiotikis’. Kwa mwaka 2000-2010 matumizi yadawa za antibiotiki yaliongezeka kwa  asilimia thelathini (30%). Pia,tafiti hizo zinaonesha kuwa kwa mwaka 2010 jumla ya tani 63,200 zaantibiotiki zilitumika kwa mifugo peke yake.

Dawa hizo zinatumika vibaya, ambapo inakadiriwa kuwa  asilimia 20-50 ya antibiotiki zinatumika isivyo sahihi duniani.

Hapa nchini Tanzania, Utafiti uliofanywa na Wizara mwaka 2014 katikamikoa  ya  Dar   es   Salaam,  Kilimanjaro,  Mbeya   na   Mwanza  ilioneshamatumizi makubwa ya dawa za antibiotiki hadi kufikia  asilimia 67.7.Pia,  

tafiti   zimebainisha   kuongezeka   kwa   kiwango   cha   usugu   waantibiotikisi. Mfano, utafiti wa kitaifa uliofanyika juu ya usugu wa dawaza   kifua   kikuu   (MDR-TB)   ilionesha   usugu   wa   dawa   kwa   wagonjwawapya kuwa ni  asilimia 1.1; na kwa wagonjwa wanaorudia dawa zaTB baada ya kupona kuwa na usugu wa asilimia 3.9. Pia, katika kutibuugonjwa   wa   malaria,   usugu   wa   dawa   za   Chloroquine   naSulfadoxine/Pyrimethamine, au “SP” ulijitokeza na kupelekea kutumikakwa dawa ya sasa iitwayo Artemether/Lumefantrine, au “ALU”. 




Katika   tafiti   ya   kutibu   maambukizi   ya   njia   ya   mkojo   (Urinary   TractInfection,   au   “UTI”)   kwa   kutumia   dawa   ya   sindano   ya   gentamycinuliofanyika katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ilionesha kuongezekakwa usugu wa dawa hiyo kutoka asilimia 6.9 mwaka 2003 hadi asilimia44   mwaka   2011.  Aidha,   katika   kutibu   ugonjwa   huo,   tafiti   nyingine1
ilifanyika   katika   hospitali   ya   Rufaa   ya   Kanda   ya   Bugando,   ambapoimeripotiwa   kuongezeka   kwa   usugu   wa   dawa   ya   sindano   yaceftriaxone kutoka asilimia 14 mwaka 2009 hadi asilimia 29.4 mwaka2011.


SABABU ZINAZOCHANGIA TATIZO HILI.
Zipo   sababu   nyingi   zinazochangia   uwepo   wa   usugu   wa   dawa   zaantimicrobials.   Mojawapo   ni   maduka   mengi   ya   dawa   kuuza   kwawananchi dawa za antimicrobials bila cheti cha daktari au kutotoa dozikamili. Ikumbukwe kuwa dawa  za  antimicrobials  hutolewa  kwa  cheticha daktari tu

Wakati   mwingine   dawa   za   binadamu   hutumika   kutibia   wanyamakinyume na sheria za matumizi ya dawa. Pia wapo wafanyabiasharawanaoandaa   vyakula   vya   wanyama   ambao  wamekuwa   na   tabia   yakuongeza  antimicrobials  kwenye   vyakula   hivyo   kwa   kufikiria   kuwazinasaidia mnyama husika kukua haraka na kutopata magonjwa.
 
  Madhara  yanayoweza   kutokea   kutokana   na   usugu   wa   dawa   zaantimicrobials  ni   pamoja   na  magonjwa   kushindikana   kutibiwa   nadawa hizo na hata kuweza kusababisha vifo. 

 Matibabu mbadala baada ya dawa za kawaida kuwa sugu yanakuwana gharama kubwa na ya muda mrefu. Mfano, matibabu ya mgonjwampya wa Kifua Kifuu kwa dawa za kawaida yanafanyika kwa kipindicha miezi sita na yanagharimu takribani shilingi laki nne (400,000/=).

Ikitokea   mgonjwa   huyo   akapata   kifua   kikuu   sugu   matibabu   hayoyanatibiwa kwa miezi 20 hadi 22 na gharama zake ni takribani shilingimilioni kumi na saba. Kama mgonjwa huyo atapata kifuu kikuu SuguZaidi   matibabu   yake   yanakuwa   ya   muda   mrefu   zaidi   na   gharamakubwa takriban shilingi milioni 64.

Watanzania wanashauriwa kuacha mazoea ya kununua dawa ovyobila   kupata   cheti   cha   Daktari  na  ushauri   wa   wataalamu  wa   afya.Ndugu wananchi, vile vile nasisitiza ni muhimu sana kumaliza dozi zadawa.

 Kila mmoja wetu ana mchango mkubwa katika kuzuia uwezekano wavimelea kujenga usugu dhidi ya dawa za antimicrobials. Mapambanodhidi ya usugu wa dawa za antimicrobials yatafanikiwa tu pale ambapomimi na wewe kwa ujumla tutashiriki katika vita hii.

“Fuata ushauri wa wataalam wa afyakabla ya kutumia antibiotiki”

Post a Comment

No comments