Friday, 3 November 2017

Homa Ya Ini: Hepatitis C



hepatitis B

Baada ya kujadili kuhusu hepatitis A na B katika kurasa zilizotangulia, leo tutaona aina nyingine ya homa ya ini, Hepatitis C. Kama ilivyo kwa hepatitis A na B, ugonjwa huu husababishwa na aina nyingine ya kirusi aitwaye Hepatitis C virus (HCV). Ni vigumu kwa kinga za mwili kuuondoa ugonjwa huu, hivyo ugonjwa huu mara nyingi huwa ni wa muda mrefu (chronic). Asilimia 85 ya watu wanaopatwa na hepatitis C, wanashindwa kuuondoa kwa kinga zao za mwili.

Baada ya muda mrefu, ugonjwa huo huharibu kabisa maini na kusababisha yashindwe kabisa kufanya kazi. Kitu kibaya ni kwamba virusi hawa wakiingia mwilini, hakuna dalili zo zote za awali zitakazojitokeza.
Kirusi wa hepatitis C hana uhusiano kabisa na virusi wengine wanaosababisha homa ya ini, kama hepatitis virus A au hepatitis virus B. Kirusi wa hepatitis C anatoka kwenye familia ya virusi ya Flaviviridae. Virusi wengine kutoka kwenye familia hii ni wale wanaoleta magonjwa ya homa ya manjano na dengue.
Uwepo wa virusi wa hepatitis C mwilini huzishtua kinga za mwili zianze kufanya kazi na hivyo uvimbe hutokea. Baada ya miaka kumi, ishirini au zaidi, uvimbe huu huweza kujenga makovu (cirrhosis). Maini yakisha fikia kuwa na cirrhosis yanaweza kushindwa kufanya kazi zake inavyopaswa hali inayoweza kupelekea madhara makubwa na hata kifo. Na, maini yenye cirrhosis yanaweza kupata saratani kwa urahisi zaidi.

Dalili Za Hepatitis C


Asilimia 75 ya wagonjwa wa hepatitis C hawapati dalili zo zote wanapoambukizwa HCV. Asilimia 25 inayobakia wanaweza kuona dalili zifuatazo:
. uchovu
. kukosa hamu ya kula
. maumivu ya misuli
. homa

Mara chache mgonjwa ataona mabadiliko ya rangi ya ngozi au macho (kuwa njano) kwenye hatua hii.
Baada ya muda, mgonjwa ataanza kuona matokeo ya kuwa na uvimbe wa muda mrefu uliotokana na kinga za mwili kujaribu kuwaondoa virusi wa hapatitis C. Wakati cirrhosis ikijijenga, mgonjwa anaweza kuona yafuatayo:
. udhaifu wa mwili
. kukosa hamu ya kula
. kukonda
. maziwa kukua kwa wanaume (gynecomastia)
. vipele kwenye viganja
. damu kutoganda upesi ukiumia

Maini hatimaye hushindwa kuendelea kufanya kazi cirrhosis ikikomaa, hali ambayo ni hatari kwa maisha ya mgonjwa. Mgonjwa anaweza kuchanganyikiwa au kuzirai (coma) kwa vile maini yatashindwa kuondoa baaadhi ya sumu nje ya mwili.
Kuongezeka kwa msukumo wa damu kwenye mishipa ya damu ya maini (portal hypertension) kunaweza kusababisha maji kujaa ndani ya tumbo na hatimaye kupelekea kuvimba kwa veni za kwenye koromeo ambazo zitachubuka kirahisi na kusababisha damu nyingi kuvuja. Kuongezeka huku kwa msukumo wa damu kwenye mishipa ya maini kunaweza kusababisha figo kufeli au kuvimba kwa bandama.
Pamoja na kusababisha damu ishindwe kuganda kwenye majeraha, hepatitis C iliyokomaa hufanya rangi ya ngozi na macho kugeuka na kuwa njano (jaundice) kwa sababu maini hayawezi tena kuondoa mchanganyiko wa vitu vya njano (bilirubin) unaotokana na chembe chembe nyekundu za damu zilizozeeka.

Hepatitis C Inaenezwaje?


Njia kuu ya kuenea kwa hepatitis C ni kupitia damu yenye virusi wa hepatitis C:
. Kuchangia sindano baina ya watumiaji wa madawa ya kulevya
. Kuchomwa sindano na wahudumu wa afya ambazo kwa bahati mbaya hazikuwa salama
. Mtoto kupata ugonjwa huu kutoka kwa mama yake anapozaliwa
. Kujamiiana bila kutumia kinga
. Kutumia vifaa vya kutobolea ngozi visivyo salama

Tiba Ya Hepatitis C


Virusi wa hepatitis C wapo wa makundi madogo tofauti yapatayo 6 na kila kundi lina usikivu tofauti kwa aina ya tiba itakayotolewa. Hali hii huifanya tiba ya hepatitis C kuwa na changamoto kwani inatakiwa uchunguzi wa kina kufanyika ili kujua aina halisi ya kirusi aliyo nayo mgonjwa ili apewe tiba anayostahili.
Kwa miaka mingi mchanganyiko wa sindano za interferon na vidonge vya ribavirin umekuwa ukitumika. Tiba hii imekuwa na mafanikio kwa karibu asilimia 60 tu ya wagonjwa. Tiba hii pamoja na kuwa haipatikani kwenye baadhi ya nchi, watu wengi wanaopata tiba hii hawamalizi dozi.
Maendeleo ya kisayansi yamewezesha kugundulika kwa dawa mpya ambazo tayari zimepasishwa na FDA na nyingine bado zinaendelea kugunduliwa, dawa ambazo wagonjwa wanaweza kuvumilia kuzitumia. Mfano wa dawa hizi ni mchanganyiko wa Telaprevir na boceprevir, Sofosbuvir (iliyopasishwa 2013) na Ledipasvir ya 2014.
Katika ukurasa wa mwisho wa mfululizo wa mada yetu ya ugonjwa wa homa ya ini, tutajadili homa ya ini ya hepatitis D na hapatitis E.

2 comments:

  1. I do not know if you would be interested in my case.Here is Dr Itua Contact Information,drituaherbalcenter@gmail.com Or mobile +2348149277967 He talk on Whatsapp too.
    I was treated for Hepatitis C genotype 2 commencing on january 14, 2017 I was treated with Dr Itua Herbal Medicine which he prepared and send to me Via EMS Courier service and I received it @ Ohio Post Office .I drink in two weeks as he instructed me to and I was cured.Just in two weeks,Isn’t that joyful.yes i’m happy and my heart fill with joy.
    I carry a high risk of Lymphoma relapse due to constant exposure to the hepatitis C virus.
    In order for me to have the maximum chance of a cure from my Non-Hodgkins Lymphoma the Hepatitis C must be treated in a timely manner or my life hangs in jeopardy. Dr Itua made my life meaningful again.And to my friend Nicky who directed me to Dr itua herbal center i forever debted to you my dear friend.Doctor Itua Assured me he can as well cured the following desease,HIV,COPD,DIABETES,HERPES VIRUS,HEPATITIS,

    ReplyDelete
  2. Regardless of whether you receive daily oral or future injectable storage treatments, they require medical service visits for drug therapy and safety and response monitoring. If patients are treated early enough, life expectancy is close to normal as long as successful treatment continues before too much immune system damage occurs. However, when patients stop treatment, the virus returns to higher levels in most patients, sometimes associated with severe illnesses, because I have passed through it and even increased the risk of death. The aim of orum treatment acı is continuing, but I think that my government has made millions of ARV drugs instead of finding a cure. for ongoing therapy and monitoring. ARV alone cannot treat HIV because it is a very long-lasting CD4 memory cell between infected cells and possibly other cells that act as long-term reservoirs. HIV can be hidden in these cells without being detected by the body's immune system. Therefore,Even if ART completely blocks the subsequent infection rounds of the cells, infected reservoirs continue before treatment is initiated, and HIV from these reservoirs returns if treatment is stopped. Ebilir Treatment ”may mean a cure for destruction, which means that HIV can remain in reservoir cells but is spiked to high levels, prevented after cessation of treatment, completely eliminating a reservoir virus body or a functional HIV treatment. Believes that Parkinson's disease is a hope for people suffering from Schizophrenia, Cancer, Scoliosis, Fibromyalgia, Fluoro-Toxicity
    Syndrome Fibrodysplasia Ossificans Progressiva.Fatal Familial Insomnia Factor V Leiden Mutation, Epilepsy Dupuytren's Disease, Desmoplastic small-round cell tumor Diabetes, Celiac disease, Creutzfeldt-Jakob disease, Chronic Fatigue Syndrome, Cerebral Amidis. Alzheimer's disease, Adrenocortical carcinoma. Alma, Allergic diseases.Hiv_ Aids, Herpes, Inflammatory bowel disease, Copd, Diabetes, Hepatitis, Tasha and I've read online how to treat Tara, so I talked to him via drituaherbalcenter@gmail.com . whatsapps +2348149277967 I believe it was easy for two weeks I drank herbal remedies and I thought Dr Itua wasn't great. Yes it is! I thank him very much, so I'll let you know if you're suffering from a disease.





    ReplyDelete