Kabla sijaongelea mada ya leo FIKIRIA HAYA MAMBO MAKUU MAWILI.
~Kila siku watu tunaumwa,kichwa,maumivu ya mifupa,maumivu ya hedhi nk.
Ukienda hospitali daktari atakupa dawa ya maumivu au unanunua mwenyewe
dawa kama Buscopan,diclofenac,paracentamol,diclopar nk. Dawa hizi ziko
mahususi kuondoa dalili sio chanzo cha tatizo(Symptomatic relief) na
imeandikwa uzinywe kwa ushauri wa daktari hii ikiwa na maana kuwa hii ni
dawa pia ni sumu ikitumiwa ovyo.Kama hujalike page yangu bofya like
kuna makala inakuja JINSI DICLOFENAC NA DAWA ZINGINE ZINAVYO ASILI UKUTA
WA UTUMBO WAKO NA KUPELEKEA KUPATA MAGONJWA SUGU
USHAURI:Siku zote tafuta chanzo cha tatizo sio kutibu dalili
~Hivi ukijiuliza swali umeenda kwa daktari ukifika
ukiwa unalalamika kusumbuliwa na mawazo na kukosa usingizi. Daktari
atakuambia unaumwa MSONGO WA MAWAZO na kukupa dawa ya kuodoa hiyo
depression kwa mfano ANTDEPRESANT AMITRYPTIRIN.. Sasa je ametibu kiini
cha tatizo au dalili. Ni dhahiri kuwa dawa zetu zinatibu dalili sio
kiini cha tatizo ndio mana leo hii kila ugonjwa daktari anakuambia
hautibiki. Ni dhahiri kuwa magonjwa tabia YANATIBIKA kama ukifuata
ushauri unaozingatia kuondoa kiini.
FUNGUO ZA MAFANIKIO KWA AFYA YAKO
1. KULA VYAKULA VYENYE SUKARI KIDOGO
2. KULA VYAKULA VYA NYUZINYUZI KWA WINGI
3. KULA VYAKULA VYA MAFUTA KIDOGO
Basi ningependa tujadili moja baada ya nyingine mpendwa msomaji wangu:
VYAKULA VYA SUKARI NYINGI
~Nimekuwa nikizungumza sana kuhusu vyakula vya sukari nyingi katika milo
yetu ya kila siku. Vyakula kama mikate, bina kiwango kikubwa cha sukari
hivyo vinasababisha mwili kuchovya Kichocheo cha insulin kwa wingi na
hatimaye kusababisha kiwango cha insulin kwenye damu kupanda. Insulin ni
kichocheo kizuri sana lakini kiwango cha juu husababisha yafuatayo:
~Kinahifadhi mafuta mwilini katika mfumo wa glycogen
~Kinakufanya uzeeke haraka
~Kinazuia kichocheo cha LEPTIN ambacho huenda kunasa kwenye vipokezi vya
ubongo na kutoa taarifa kuwa umetosha na kula(yani kushiba). Kuzuiliwa
kwa hiki kichocheo ndio mana watu wenye uzito mkubwa utakuta anakula
sana jua ana insulin nyingi ambayo inazuia Leptin ambayo hutoa taarifa
ya kutoshelezwa la mlo kuzuiliwa.
~Pia insulin kuwa juu kunafanya tatizo lako la uchovyaji vichocheo kuharibika.
WANAUME
~Kiwango kingi cha insulin kwenye damu husababisha uchovyaji wa
Testosterone kuzuilika hivyo kusababisha mwanaume kukosa
shauku,hamu,nguvu na hamasa ya kuelendelea na tendo la ndoa. Hivyo basi
inasemekana kwamba walaji wa vyakula hivi vya sukari mara nyingi huwa
wana kiwango kingi cha insulin kwenye damu ndio mana wana matatizo
mengine ya nguvu za kiume na mengine Kama chunusi sugu,macho kushindwa
kuona vizuri nk
WANAWAKE
~Ninapenda kusikitika kuwa ongezeko la dada zetu na mama zetu wenye
matatizo ya uzazi kama fibroids,cancer,mizunguko mibovu na maumivu
wakati wa hedhi. Sasa ningependa nikwambie nini chanzo na hatua za
kuchukua. Ulapo vyakula vya sukari nyingi vinakufanya kiwango cha
INSULIN kuongezeka kuja kusawazisha sukari hiyo mwilini. Kuongezeka kwa
insulini kunafanya uchovyaji wa ESTROGEN KUWA JUU na kushusha kiwango
cha PROGESTERONE. Hiki tunasema HORMONAL IMBALANCE. Kuongezeka kwa
kichocheo hiki kunasababisha yafuatayo:
~Estrogen ni mbolea nzuri sana ya vimbe mbalimbali mwilini mwako yan
ESTROGEN DEPENDANT TUMORS kama FIBROIDS uvimbe kwenye kizazi,Kansa ya
titi au uvimbe wa titi,Kansa ya shingo ya kizazi nk. Ni dhahiri kuwa ni
changamoto kubwa namna au njia rahisi ya kutibu hili tatizo ni
kusawazisha kiwango cha hormone na kuondoa uvimbe kwa operation.
Unapofanyiwa operation haimanishi chanzo cha tatizo ambalo ni kiwango
cha juu cha hormoni kimerekebishwa. Mbolea itabaki pale pale na wagonjwa
wengi wanaofanyiwa operation ya kuondoa kiuvimbe na kuacha
kizazi(myomectomy) hurudia tena uvimbe huo baada ya muda mfupi. CHANZO
NI KULA VYAKULA HIVI VISIVYO NA FAIDA MWILINI BALI NI KUJIONESHA UFAHARI
WA PESA.
~Pia kwa dada zangu wenye maumivu makali ya hedhi ambayo hupelekea
kupata kichefuchefu,tumbo kuuma,mgongo kuuma,kuharisha,msongo wa
mawazo,kula sana,na kuchoka sana bila kusahau hasira sana. Hii ni
kutokana na kiwango cha juu cha insulin ambacho kufanya kiwango cha
estrogen kuwa juu na progesterone kushuka hivyo kupelekea maumivu hayo.
Matibabu ya hili tatizo ni changamoto pia, Utumiapo dawa za maumivu kama
DICLOFENAC,BUSCOPAN,IBUPROFEN utafiti unaonesha kuwa zinaweza kupelekea
ukapata tatizo jingine sugu ambalo ni kali zaidi ya hilo mwanzo huitwa
PREMENSTRAL DYSPHORIC DYNDROME. Maumivu huongeza muda wake na yanakuwa
makali kadri siku zinavyo enda. Hivyo utumiapo hizo dawa huondoi tatizo
bali unazidi kuongeza usugu wa tatizo. Tiba ni kujua na kuepuka vyakula
vibaya vyenye sukari nyingi na kurekebisha mwenendo wa maisha yako
INAENDELEA UFUNGUO WA PILI.....BOFYA LIKE PAGE YANGU UENDELEE KUPATA MAKALA ZANGU ZA AFYA.
No comments
Post a Comment